Wednesday 27 November 2013

B'Hits yajibu madai ya Mabeste kudhalilishwa na kuondoka kwa wasanii.

Siku moja baada ya Mabeste kusikika kupitia chombo kimoja cha habari akidai kudhalilishwa na maelezo yaliyotolewa na C.E.O wa B’Hits Hermy B kuwa msanii huyo amekosa shukrani kwa kuwa alikuwa akisaidiwa na kampuni hiyo kulipia pango la nyumba na mambo mengine kama ndugu.

Uongozi wa B’Hits kupitia COO (Chief Operations Officer) ambaye pia ni mwana sheria Amani Joachim, ameyatolea maelezo ya kina malalamiko hayo kupitia kipindi cha Bongo Dot Home cha 100.5 Times fm.

Amani
Lakini pia kiongozi huyo wa B’Hits amefunguka hali halisi ya mambo yalivyo kutokana na jinsi ambavyo baadhi ya watu wamekuwa wakijiuliza kwa nini wasanii wanaondolewa B’Hits kunzia wale wa mwanzo hadi hawa walioondolewa hivi karibuni (Vanessa, Mabeste na Gosby).

www.thefameshow.blogspot.com

No comments:

Post a Comment